Posts

Showing posts from April 7, 2017

Alichokiandika Mbunge Hessein Bashe kuhusu Roma Mkatoliki.

Alichokiandika Mbunge Hussein Bashe kuhusu Roma Mkatoliki By Rama Mwelondo . TZA . Usiku wa April 5 2017 taarifa za kukamatwa kwa msanii wa hip hop Roma Mkatoliki zilianza kuenea katika mitandao ya kijamii kwa kuripotiwa kuwa Roma Mkatoliki na Moni wakiwa Studio za Tongwe Records walikuja kukamatwa na watu wasiojulikana na kuwapeleka kusikojulikana. Watu mbalimbali ikiwemo wasanii mbalimbali wamekuwa wakionesha hisia zao juu ya tukio hilo kwa kutumia kurasa zao za mitandao ya kijamii kuoneshwa kuguswa na tukio hilo, Mbunge wa Nzega Hussein Bashe ni miongoni mwa watu waliyotumia kuraza zao za instagram kuandika anachowaza kuhusu Roma. Who is behind all this? “ Ni genge ambalo limejipa mamlaka ya kupandikiza woga na chuki miongoni mwa jamii na kuharibu Taswira ya CCM. Tunawajibu wa kukataa woga ,Tunawajibu wa kutoruhusu Misuse ya vyombo vya Ulinzi na usalama, Tunawajibu wa kulinda Taifa letu ” “ Tunawajibu wa kupigania Values zilizopiganiwa na waasisi wa Taifa letu kama Mzee

Maneno Matatu ya Nape Kuhusu kutokuonekana kwa Roma.

Maneno matatu ya Nape Nnauye kuhusu Roma . Baada ya mastaa mbalimbali kuguswa juu ya stori ya Roma mkatoliki na wenzake watatu kuchukuliwa na watu wasiofahamika kwenye Studio za Tongwe Records na kupelekwa sehemu isiyojulikana, sasa leo April 7 2017 Mbunge wa Mtama (CCM) Nape Moses Nnauye ameonesha hisia zake juu ya tukio hilo. Kupitia account yake ya twitter Nape Nnauye ameyaandika maneno haya matatu kuhusu Roma…>>> ”Roma! Oooooh No! ” -Nape Nnauye.

The Siti Msanii kutoka TONGWE alivyoshuhudia kuchukuliwa kwa Roma.

Shuhuda ameeleza Roma na wenzake walivyochukuliwa Tongwe Records. Zimepita siku mbili tangu staa wa Hip Hop Bongo Roma kuchukuliwa na watu wasiojulikana pamoja na wenzake wakiwa katika studio za Tongwe Records bila kujulikana walikopelekwa, basi leo April 7, 2017 msanii kutoka Tongwe Records ameelezea jinsi watu hao walivyochukuliwa. The Siti ameiambia millardayo.com na Ayo TV jinsi Roma Mkatoliki na wenzake walivyochukuliwa Tongwe Records ambapo hadi sasa haijafahamika mahala walipo na watu waliowachukua . Akizungumza na millardayo.com pamoja na  Ayo TV The Siti alisema:>>> ”Ilitokea kama Jumatano saa kumi na mbili jioni na walikuja watu pale wakashuka kutoka kwenye Noah wakatuambia tuingie ndani ya geti na tukaingia ndani ya geti. Wakamuulizia Junior wakaambiwa hayupo, kisha wakamuulizia na Roma Mkatoliki wakaomba waitiwe Roma kisha walipoitiwa Roma, walimuhoji pale mara wakaingia studio wakachukua vitu na wakawachukua wakina Moni .” -The Siti.

Taarifa iliyotolewa na Wizara ya Habari,Sanaa na Michezo Kuhusu Roma.

Taarifa ya kwanza ya Wizara ya Habari kuhusu kupotea kwa Roma Mkatoliki. Taarifa za kupotea kwa Msanii Roma Mkatoliki na wenzake watatu baada ya kutekwa na kuchukuliwa na Watu wasiojulikana kwenye studio za TONGWE Dar es Salaam, zilianza kusambaa kuanzia juzi usiku (April 5 2017). Leo April 7 2017 Wizara ya Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo ambayo iko chini ya Dr. Mwakyembe imetoa taarifa ifuatayo >>>> “Kwa dhamana yake katika tasnia ya Sanaa, Wizara imepokea kwa mshtuko taarifa za kutoweka kwa Mwanamuziki Ibrahim Mussa kwa jina la kisanii “ Roma Mkatoliki ””. " Wizara imefuatilia kwa karibu suala hili kwa kuwa lina muelekeo wa jinai. Hata hivyo taarifa kutoka vyombo vya dola zinathibitisha kuwa Roma Mkatoliki hashikiliwi katika kituo chochote cha polisi ." Kutokana na hali hiyo, Wizara inawaomba wadau mbalimbali na wananchi kwa ujumla kushirikiana na Jeshi la Polisi kwa kutoa taarifa zozote zitakazo saidia kujua alipo msanii huyo.

Maneno ya Nchemba Kuhusu Roma.

Maneno 39 ya Waziri Nchemba kuhusu Roma Mkatoliki . Usiku wa April 5 2017 taarifa za kukamatwa kwa msanii wa hip hop Roma Mkatolikia zilianza kuenea katika mitandao ya kijamii kwa kuandikwa kuwa Roma Mkatoliki na Moni wakiwa Studio za Tongwe Records walikuja kukamatwa na watu wasiojulikana na kuwapeleka kusikojulikana. Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mwigulu Nchemba ambaye ndio anahusika na usalama wa raia, ametumia ukurasa wake wa Instagram kuonesha kuguswa na tukio la kutekwa kwa Roma Mkatoliki na Moni , Waziri Nchemba ameeleza kuwa amewaagiza polisi kufuatilia na kutoa taarifa kwa umma. “ Nimeshtushwa kwa kutokuonekana kwa Msanii Roma na Wenzake mpaka sasa. Nimeshtuka zaidi nilipofuatilia na kuambiwa hakuna kituo chochote cha polisi kinachowashikilia. Nimeelekeza Polisi wafuatilie kwa karibu kujua undani wa tukio hili na hatima yao na kutoa taarifa kwa umma ” -Nchemba.

Wanasayansi wamegundua Tiba ya Hangover.

Utafiti Mpya kutoka kwa Wanasayansi, wamegundua tiba ya Hangover Hii ni dunia ambayo kila siku watu wanafanya utafiti wa mambo mbaimbali…sasa leo April 7, 2017 nakuletea matokeo ya utafiti uliofanywa na wanafunzi wa wawili nchini Marekani waliogundua tiba ya hangover. Unaambiwa katika stori iliyochapishwa na Daily Mail March 29, 2017, wanafunzi wawili kutoka Yale University wamegundua tiba hiyo ambayo wameapa jina la SunUp ikiwa ni unga uliotokana na mchanganyiko wa viungo vya asili ambao umegunduliwa kwa lengo la kuvunja vunja molikuli za sumu kwenye ini, na kubalansi glutamine pamoja na kuuamsha mwili kwa elektroliti baada ya kunywa pombe. Margaret Morese na Liam McClintock ambao waliathiwa sana na Hangover waligundua tiba hiyo baada ya kujaribu viungo vya asili kila kimoja kivyake katika tafiti huru kuthibitisha uwezo wake dhidi ya kuondoa athari za kilevi na ulinzi thabiti dhidi ya sumu itokanayo na kilevi kwa mtumiaji na baadaye kutengeneza unga huo ambao humtaka mtumiaj

Taarifa Kuhusu Kupotea Kwa Msanii Roma Mkatoliki.

Taarifa zilizopo ni kuwa Msanii Roma Mkatoliki kutokea katika Studio ya Tongwe ( Tongwe Rocords ) alivamiwa na watu wasiojulikana Majira ya Usiku wa kuamkia Siku ya Alhamisi. Msanii huyo alivamiwa Studioni hapo akiwa  studioni hapo na kupelekwa sehemu kusilojulikana pamoja na mwemzake Moni au @ centralzone kama anavyojulikana. Familia ya Msanii Roma ( Mkewe ) ameweza kusema kuwa simu ya Msanii huyo(Mmewe) imekuwa ikiita tu bila kupokelewa hivyo akiwaomba Watanzania wote waweze kumpa ushirikiano wa taarifa zozote za kuhusiana na Msanii Roma (Mmewe) sehemu yoyote ile ambapo zlatapatikana.

Nay Wa Mitego Ametusogezea Wapo video.

Bofya hapa chini kuitizama. http://millardayo.com/po67/