Posts

Showing posts from April 10, 2017

Viwanja Kumi Bora Afrika,Ukanda wa Mashariki Upo mmoja tu.

TOP 10 ya viwanja ghali zaidi Afrika , Afrika Mashariki upo mmoja . Licha ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Africa CAF kusema moja ya sababu kuu inayopelekea Bara la Africa kufanya vibaya kwenye mchezo wa mpira wa miguu duniani ni ukosefu wa viwanja bora, kuna baadhi ya nchi Afrika zina viwanja vizuri na vyenye gharama kubwa ukilinganisha na nchi nyingi zilizoendelea. Leo April 10, 2017 nimekuletea list ya viwanja 10 vizuri na vyenye gharama zaidi barani Afrika hadi kufikia December 2016. 1: Capetown Stadium, Afrika Kusini Uwanja huu una uwezo wa kuingiza mashabiki 64,100 ambapo umejengwa na kampuni ya Afrika Kusini ukiigharimu nchi hiyo Dollar 600 million ukiwa ndiyo uwanja wenye gharama kwa Afrika. 2: Moses Madiba Stadium, Afrika Kusini Moses Madiba ulikuwa moja ya viwanja vilivyotumika wakati wa Fainali za Kombe la Dunia 2010 ukiwa na uwezo wa kuingiza mashabiki zaidi ya 62,760. Uligharimu Dollar 450 million. 3: FNB Stadium, Afrika Kusini Uwanja huu unashikilia rekodi ya

Tamko la Waziri Kuhusu Bonde la Mto Ruaha.

Tamko la waziri Makamba kuhusu bonde la Mto Ruaha . Jumapili ya April 9 2017 waziri wa nchi ofisi ya makamu wa Rais-muungano na mazingira January Makamba aliamua kufanya mkutano na waandishi wa habari na kueleza mpango wake wa kuzindua kikosi kazi cha kitaifa kuhusu bonde la M to Ruaha mkuu Iringa . Mpango huo ambao makamu wa Rais na mawaziri watano wataelekea Iringa siku ya Jumanne ya April 11 2017 lengo likiwa ni kukagua na kuangalia bonde la mto Ruaha ambalo linakabiliwa na uharibifu mkubwa wa mazingira hususani wa ardhi. Uharibifu wa mazingira katika bonde la mto Ruaha kwa kiasi kikubwa unatokana na shughuli za kibinadamu zisizo endelevu zinazofanywa katika maeneo ya vyanzo vya maji pamoja na vilele vya milima, miteremko ya milima na katika mabonde. Baada ya kugundua uharibifu huo unaoendelea kufanyika katika bonde la mto Ruaha, serikali kwa kushirikiana na wadau imeona kuna haja ya kuwa na mtazamo mpya wa namna ya kukabiliana na changamoto za mto Ruaha Mkuu kwa ufa