Posts

Showing posts from April 4, 2017

Mapato yalikusanywa na TRA ndani ya Miezi Tisa.

Mapato ambayo TRA wamekusanya kwa miezi Tisa. Mamlaka ya Mapato Tanzania ‘TRA’ imetoa ripoti ya mapato yaliyokusanywa ndani ya miezi 9 kuanzia June 2016 hadi March 2017 ambayo ni Shilingi Trillion 10.87 ikiwa ni ongezeko la asilimia 9.99 ukilinganisha na mwaka uliopita. Akizungmzia makusanyo hayo Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipa Kodi Richard Kayombo alisema zaidi ya Shilingi Trillion 1.34 zilikusanywa katika mwezi March 2017 pekee ikionesha kupanda kwa asilimia 2.23 ukilinganisha makusanyo ya mwezi kama huo mwaka 2016 ambapo zilikusanywa Shilingi Trillion 1.31.