Posts

Showing posts from April 6, 2017

Stori Kumi za Uharifu Zitakazokushangaza Zaidi.

Stori Kumi(10) za wahalifu zitakazokushangaza duniani. Wahalifu wengi hutumia akili nyingi wakati wa kufanya uhalifu ili wasikamatwe au kutiwa nguvuni na vyombo vya dola lakini mara nyingine hujikuta wamefanya makosa madogo madogo ambayo huwakamatisha na kujikuta mikononi mwa sheria. 1: Joseph Martin  Joseph Martin kutokea Florida Marekani alipiga simu Polisi kushitaki baada ya kuagiza bangi na muuzaji kukimbia na pesa yake. Badala ya Polisi kumsaidia shida yake walimtafuta na kumkamata kwa kosa la kutumia mihadarati ambayo imezuiwa kisheria. 2: Tyron Jr Tyron Jr kutokea Carlifornia Marekani alikwenda Mahakamani kusikiliza kesi yake ya wizi wa gari lakini alijikuta akipata kesi mbili baada ya Polisi kugundua gari aina ya Lexus SUV alilokuja nalo Mahakamani hapo aliliiba miezi michache iliyopita kabla ya kukamatwa kwa kesi ya pili. 3: Jonathan Parker Jonathan Parker alivamia nyumba moja katika mji wa Pennsylvania Marekani ambapo baada ya kuiba vitu kadhaa aliamua kuingia kwenye