Posts

Showing posts from April 3, 2017

Wasanii Waliowahi Kuambiwa hawajui kuimba lakini sasa ni Mastaa.

BURUDANI Waimbaji 10 waliowahi kuambiwa hawajui kuimba lakini leo ni mastaa wa Dunia. Mara nyingi watu wanaposhindwa na jambo hukata tamaa lakini kushindwa mara moja haimaanishi huwezi kufanikiwa jambo hilo ukijaribu tena na tena, leo nimekuletea list ya wanamuziki kumi waliowahi kuambiwa hawajui kuimba na leo hii ni mastaa wakubwa duniani. 1: Beyonce . Akiwa na miaka 14 tu alipelekwa na baba yake Mathew Knowles studio lakini producer alipomsikia Beyonce akiimba alimwambia hadhani kama kuimba ni kipaji chake lakini leo hii Beyonce ni miongoni mwa waimbaji wakubwa duniani akiwa na thamani ya zaidi ya dola za kimarekani Milioni 600 na kuuza zaidi ya rekodi milioni 34. 2: Shakira . Shakira ni miongoni mwa waimbaji wenye mafanikio makubwa dunia akiwa na thamani ya zaidi ya dola milioni 220 na kuuza rekodi  zaidi ya milioni 60 duniani kote lakini aliwahi kukataliwa kujiunga na kikundi cha kuimba kwaya kanisani na mwalimu wake wa muziki kumwambia ana sauti mbaya inayofanana na mbuzi. 3

Mfahamu Millard Ayo.

Huyu ndiye @ millardayo . com Mtangazaji wa Radio na Televisheni unayemtazama na kumsikiliza kila siku. Kwa Majina anaitwa Millard Afrael Ayo alizaliwa mkoanni Arusha January 26 akiwa ni mtoto wa kwanza kwenye famili ya watoto wanne ya Afrael Ayo ambae ni mmeru wa Akheri Tengeru, ni mfanyabiashara na mama Mary Ayo ni mwalimu. Baada ya mama yake mzazi kuona uharaka wa uelewa wa Millard, alimuanzisha shule akiwa mdogo sana na hatimae kumaliza elimu ya msingi akiwa na miaka 12 tu, akamaliza form four akiwa na miaka 16 mwaka 2002, sehemu zote hizo yeye ndio alikua mdogo kuliko wote darasani kuanzia Patandi Primary School Tengeru, Akeri Secondary School na Mbezi Beach High School. Wakati akisubiri majibu, Millard alijiunga na Arusha College of Electronics na kusomea ufundi wa kutengeneza satelitte dish, tv deck na radio masomo ambayo aliyamaliza na aliyasoma kwa sababu ilikua ni kazi ya pili aliyoipenda, baada ya hapo mama yake mzazi alishawishiwa na marafiki zake ili Millard

Manyanyaso kwa mtoto husababisha kuwahi Kubarehe Mapema.

DUNIANI UTAFITI: Manyanyaso kwa mtoto husababisha kubalehe mapema. Wataalamu wa Saikolojia kutoka Chuo Kikuu cha Penn State, Marekani wamegundua katika utafiti wao kuwa zaidi ya 90% ya watoto waliopitia maisha ya kunyanyaswa, kupigwa au kudhalilishwa kingono wanabalehe haraka ukilinganisha na watoto wanaolelewa kwa upendo. Professor Jennie Noll aliliambia Jarida la Adolescent Health: >>> “Watoto hasa wa kike wanaolelewa kwa kunyanyawa hasa kupigwa au kubakwa hubalehe kabla ya muda ukilinganisha na watoto wanaolelewa kwa upendo pia watoto wa aina hii huota matiti mapema ukilinganisha na watoto wa kawaida.“ Akielezea uhusiano ulipo baina ya mtoto kunyanyaswa na kubalehe kabla ya wakati Dr. Noll alisema watoto wanaokuwa katika mazingira kama hayo huzalisha homoni nyingi zinazotokana na msongo mkubwa wa mawazo hivyo kuharakisha muda wa balehe. Wanasaikolojia hao pia walisema mtoto anayenyanyaswa yuko hatarini zaidi kupata saratani ya ovari na matiti ukilinganisha na watoto a

Nusu ya Wamarekani wahitaji Donald Trump aondelewe.

DUNIANI Nusu ya Wamarekani wataka Donald Trump aondolewe madarakani. Taasisi ya utafiti ya sera za umma Marekani imetoa matokeo ya utafiti uliofanywa February 2017 kuhusu utendaji kazi wa Rais wa nchi hiyo ambapo  zaidi ya nusu ya Wananchi wameonesha kumkataa Donald Trump huku zaidi ya asilimia 44 wakilitaka Bunge la nchi hiyo kupiga kura za kumuondoa madarakani. Kwa mujibu wa utafiti huo asilimia 44 ya watu wamejutia kumchagua Donald Trump baada ya kufuta sera ya afya iliyoanzishwa na Rais Obama “Obamacare” bila kuweka sera mpya huku asilimia 44 walisema ni mtu asiye muaminifu na asilimia 64 wakimtaka Rais huyo kuonesha hadharani mlolongo wake wa ulipaji kodi. Utafiti huo pia umeonesha Donald Trump anashika namba tatu kati ya wanasiasa wanaochukiwa na wananchi kwa sasa huku akiongozwa na Msemaji Mkuu wa Bunge Paul Ryan.

Taarifa Kuhusu Mgomo wa Mabasi.

Taarifa kuhusu mgomo wa mabasi kesho. Mgomo wa usafirishaji wa abiria na mizigo usio na kikomo uliopangwa kufanyika kuanzia kesho April 4 2017 na chama cha wamiliki wa mabasi na malori nchini sasa umesitishwa, mgomo huo ulikuwa unapinga sheria zilizotungwa na Mamlaka ya usafiri wa nchi kavu na majini ‘SUMATRA’ ambazo zinatajwa kuwa na vifungu amabvyo ni kandamizi vinavyoweza kutishia ustawi biashara ya mabasi nchini. Mgomo huo umesitishwa baada ya wamiliki hao kukutana na Waziri wa Mawasiliano, Ujenzi na Uchukuzi Prof. Makame Mbarawa na SUMATRA na kufikia makubaliano kwa yale ambayo walikuwa wameyataka yafanyiwe marekebisho.

Nchi 21 Duniani ambazo Raia wake siyo Walarimu.

Nchi 21 Duniani ambazo Raia wake siyo wakarimu, Afrika imetajwa nchi moja tu. # millardayo. Watafiti kutoka Chuo Kikuu cha Wroclaw Poland wametoa list ya nchi zenye wananchi wasiokuwa wakarimu duniani ambapo Romania imeshika namba moja ikifuatiwa na Hungary ambapo kwa mujibu wa utafiti huo watu wa Romania wanaongoza duniani kwa kuchukia ukaribu na mtu, kwa wastani mtu hutaka usimame sentimita 139 kutoka alipo. Katika list hii nchi pekee kutoka Afrika ni Uganda ambapo imeshika namba tano kwa kuwa na watu wasiowakarimu duniani, huku mtu akitaka usisimame karibu yake kwa sentimita 127. Tazama list ya nchi 21 duniani zenye raia wasiowakarimu duniani, stori hii ni kwa mujibu wa www.indy100.com

Wanyama wanaopewa Heshima kubwa za Kijeshi.

DUNIANI Viumbe watano wanaopewa heshima kubwa jeshini mbali na binadamu By Farhiyah Adam. Kwa kawaida wanyama hurahisisha maisha ya binadamu kwa kuwa walinzi, chakula na usafiri, lakini kuna baadhi ya wanyama na ndege walioweza kujiwekea heshima duniani hasa  kwenye sekta maalum za kijeshi na wameweza kupata nafasi za juu jeshini. 1: Sir Nils Olav Nils Olav ni ndege aina ya Penguin aliyepewa cheo mara ya kwanza mwaka 1972 na kuwekwa kwenye timu ya walinzi wa mfalme Harald V Loudon wa Norway. Kwa sasa Sir Nils Olav ni Brigedia anapewa heshima zote za kijeshi ikiwemo kupigiwa saluti na kukagua jeshi. 2: Treo Ni mbwa aliyetumikia jeshi la Uingereza kuanzia mwaka 2001 mpaka 2015. Trio ana medali zisizopungua 63 ambazo alipewa baada ya kufaya kazi kubwa ya kutegua mabomu na kutambua mahali mabomu yalipofichwa. 3: William of Orange. William ni njiwa aliyekuwa mwanajeshi wa jeshi la Uingereza mwenye namba MI14 ambapo mwaka 1944 alipewa medali ya 21 baada ya kupeleka ujumbe uliookoa v

Dawa ya Kuzuia Kuzeeka kwa Vinasaba(DNA).

DUNIANI UTAFITI: Naambiwa imegundulika dawa ya kuzuia usizeeke na inatibu kisukari. @Tza millardayo. April 2 2017 nimekutana na stori ambayo inawahusu wanasayansi kutoka Chuo Kikuu cha New South Wales Marekani kugundua dawa zitakazomzuia mtu kuzeeka, huku zikisaidia kurekebisha seli za mtu aliyezeeka na kurekebisha vinasaba ‘DNA’ vilivyoharibika ambavyo ndio sababu kuu ya uzee. Mkuu wa utafiti huo Professor David Sinclair aliiambia Science Today kuwa: >>>” Dawa hizi zitazuia uzee kwa kupambana na magonjwa yote yanayosababisha ngozi na mifupa ya binadamu kuharikibika. Itaponya magonjwa kama Kisukari, Saratani na magonjwa mengine yanayosababishwa na uzee, pia itasaidia kulinda kiwango cha mafuta mwilini ‘Calories’ na kuongeza maisha marefu ” Ripoti ya utafiti huo ilionesha jaribio la kwanza lilifanywa kwa panya mzee ambapo baada ya wiki moja kulikuwa na mabadiliko chanya kwenye ngozi na seli zake zikionekana kuimarika kwa kiasi kikubwa, huku jaribio la kwanza kwa binadamu li