Jinsi ya Kurudisha Vitu vilivyofutwa au kupotea kwenye simu yako(Data Recovery).
JINSI  YA KURUDISHA  DATA ZAKO  ZILIZOPOTEA  KWENYE  SIMU  Njia Za Kupata Data Zako Zilizopotea (Zilizofutwa) Katika Kifaa Cha Android!  Sio kitu kipya wote tumeshawahi fanya, kwa bahati mbaya tulishawahi kufuta taarifa zetu kama vile picha au hata video. Kama ikitokea hivyo tena usikasirike, TeknoKona inakuletea njia.  Sawa kama nlivyosema kuwa unaweza ukapata taarifa zako zote ambazo ulifuta kwa bahati mbaya lakini kabla ya kuzipata kuna mambo inabidi uyafanye  • Usihifadhi (save) kitu kingine chochote katika simu kifaa chako au izime mpaka ukiwa unampango wa kufufua vitu vyako  • Zima WiFi na njia  za mawasiliano  za 2G/3G ili  masashisho  (update)  ambayo  huwa  yanayofanyika automatiki yasifanyike . Kumbuka kama yakifanyika, mafaili mapya yanaweza jiweka juu ya yale ambayo unataka kutafufua  Tuifahamu Njia  Kama Mafaili  Yako Yapo  Katika  Memori  Kadi .  Ukishaona mafaili yako yamefutika bahati mbaya – au hata kwa makusudi – kitu kinachofuata ni kuunganisha...